|
Kiongozi wa Kiislamu Somalia akanusha kufanya mazungumzo na rais wa nchi hiyo
2009-05-04 21:25:45
Na EAR Habari
Kiongozi wa Kiislamu mwenye ushawishi nchini Somalia amekanusha uwezekano wa kufanya mazungumzo na rais wa nchi hiyo katika jitihada za kumaliza ghasia zilizoigubika nchi hiyo kwa miaka kadhaa.
Kiongozi hiyo Sheikh Hassan Dahiri Aweys ametoa wito kwa waislamu nchini Somalia kuendelea kupambana na serikali inayoongozwa na kiongozi mwenye msimamo wa wastani Sheikh Sharif Sheikh Ahmed.
Sheikh Aweys alirejea nchini Somalia mwezi uliopita kutoka ukimbizini huko Eritrea na kuashiria kuwepo kwa uwezekano wa yeye kufanya kazi na rais wa Somalia ambaye hapo awali walikuwa katika kambi mmoja.
|